Messi kumalizia soka Argentina

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th November 2024


Messi kumalizia soka Argentina

Kwa mujibu wa mtandao wa GOAL, Lionel Messi anataka kujiunga na timu yake ya utotoni, Newell's Old Boys, baada ya kumalizika kwa msimu wa MLS wa mwaka 2025

Inaelezwa Messi ambaye ameshindwa kuisaidia timu yake kwenda hatua ya nusu fainali ya mtoano wa ligi Ukanda Mashariki licha ya kufunga mabao 20 katika msimu wa kawaida, anachosubiria kwa sasa ni kumalizika kwa makataba wake mwisho wa msimu huu.

Kocha wa Miami, Tata Martino ameonyesha wasiwasi wa kuwa staa huyo anaweza kuondoka ingawa alishindwa kuweka wazi ni lini.

"Kwa kweli sijui ni muda gani Messi anaweza kuendelea kuwa hapa, ni kweli muda wa mkataba wake unakaribia kuisha lakini siwezi kusema yupo hapa kwa muda mfupi," alisema Martino alipokuwa akizungumzia hatma ya Messi kikosini hapo

Miami ambayo imeshindwa kufuzu kwenda hatua ya mtoano kwa ajili ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Marekani tayari imeshachaguliwa kuwa timu itakayoshiriki michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2025 itakayofanyika huko Marekani jambo lililozua malalamiko kwa timu nyingi pinzani za Marekani.

FIFA iliitangaza Miami kuwa itashiriki Kombe la Dunia kwa kigezo cha kushinda tuzo ya Supporter Shield inayotolewa na waandaaji wa Ligi Kuu ya Marekani kwa timu iliyofanya vizuri katika msimu wa kawaida na wao watakuwa ndio wenyeji

Messi na timu yake wamefanya vibaya msimu huu baada ya kutolewa katika raundi ya kwanza ya mtoano na Atalanta United.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.