Simba Queens, Yanga Princess uso kwa uso Ligi ya Wanawake

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th November 2024


Simba Queens, Yanga Princess uso kwa uso Ligi ya Wanawake

Mikiki mikiki ya Ligi Kuu ya Wanawake inaendelea ambapo ligi hiyo imeingia raundi ya nne ambapo kesho Jumatano Derby ya Kariakoo upande wa kinadada Simba Queens vs Yanga Princess itapigwa

Simba Queens ndio vinara wa ligi hiyo wakiwa kileleni mwa msimamo wakikusanya alama 9 baada ya kushinda mechi zote tatu huku watani zao Yanga Princess wakisaka ushindi wa kwanza msimu huu baada ya kulazimishwa sare katika mechi zote tatu

Kocha Mkuu wa Yanga Princess amesema licha ya kikosi chake kukosa ushindi katika mechi zilizopita lakini watakuwa tayari kuikabili Simba Queens kwani mchezo huo wanafanya maandalizi tofauti ya kimbinu

Nae kocha wa Simba Queens, Yussif Basigi amesema kuwa wachezaji wake wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo utakaopigwa katika dimba la KMC Complex, Mwenge

Basigi amesema mchezo huo utakuwa wa kuvutia, ikiwa ni mechi yake ya pili ya Derby tangu alipojiunga na Simba Queens

Simba Queens ilichapwa na Yanga Princess katika mchezo wa nusu fainali Ngao ya Jamii timu hiyo zilipokutana mwezi uliopita


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.