Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha amesema endapo timu ya Tabora United itaifunga Simba kwenye mchezo wa Ligi kuu bara utakaochezwa Desemba 28 mwaka huu basi atawazawadia motisha ya Tsh 50 Milioni
Chacha ameyasema hayo jana wakati akiwa kwenye maandalizi ya kukabidhi Tsh 20 Milioni alizowaahidi Tabora United baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi yaa Yanga





