Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha amesema endapo timu ya Tabora United itaifunga Simba kwenye mchezo wa Ligi kuu bara utakaochezwa Desemba 28 mwaka huu basi atawazawadia motisha ya Tsh 50 Milioni
Chacha ameyasema hayo jana wakati akiwa kwenye maandalizi ya kukabidhi Tsh 20 Milioni alizowaahidi Tabora United baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi yaa Yanga
Katika mchezo wa duru ya kwanza, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 uwanja wa KMC Complex
Timu hizo zitachuana tena Disemba 28 ukiwa ni mchezo wa duru ya pili utakaopigwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali ametamba kuwa Simba sio timu ya kuwekea ahadi
"Mnajisumbua tu Simba sio timu ya kuiwekea ahadi," aliandika Ahmed katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii



