Mwamuzi kutoka nchini Sudan Kusini, Ring Nyier Akech Malong ndiye ambaye ameteuliwa na Shirikisho la soka Afrika (CAF) kuchezesha mchezo kati ya Ethiopia dhidi ya Tanzania ukiwa ni mchezo wa kusaka tiketi ya kufuzu AFCON 2025
Mchezo huo utapigwa Lubumbashi DR Congo, Jumamosi Novemba 16, 2024
Stars inahitaji kushinda mchezo ili kuweka hai matumani ya kufuzu fainali za Afcon 2025 zitakazofanyika Morocco mwakani
Tanzania itakamilisha mechi ya mwisho kundi H uwanja wa Benjamin Mkapa, Novemba 19 dhidi ya Guinea
Kimahesabu kama Tanzania itashinda mechi zote mbili itaungana na DR Congo kucheza Afcon 2025