Kikosi cha Singida Black Stars kinachonolewa na kocha Patrick Aussems leo kitashuka dimba la Tanzanite Kwaraa huko Manyara kumenyana na Fountain Gate katika mchezo wa kirafiki
Mechi hiyo ya 'Derby ya ndugu', ni kwa ajili ya maandalizi ya timu zote kuelekea mechi zinazofuata za ligi kuu baada ya kuhitimishwa kwa kalenda ya FIFA
Ligi itakaporejea, Singida BS itasafiri ugenini Tabora kumenyana na Tabora United katika mchezo utakaopigwa Novemba 24 uwanja wa Ali Hassan Mwinyi
Aidha, mchezo kati ya Yanga dhidi ya Fountain Gate uliopaswa kupigwa Novemba 21, umeondolewa na utapangiwa tarehe nyingine
Singida BS inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na alama 23 wakati Fountain Gate iko nafasi ya 5 ikiwa na alama 17



