Baada ya kuichapa DR Congo bao 1-0 hapo jana, Guinea imefikisha alama 9 na kurejea katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi H
Maana yake ni kuwa Tanzania sasa lazima ishinde mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi dhidi ya Guinea Jumanne, Novemba 19 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Tanzani ambayo jana iliichapa Ethiopia mabao 2-0, imekusanya alama 7 ikiwa nafasi ya tatu, kundi H
Ni nafasi adimu kwa Tanzania kujihakikishia kufuzu kwa fainali za Afcon 2025 kwa mara ya tatu katika historia. Mchezo huu si tu fursa ya kihistoria, bali pia kipimo cha uwezo wa Stars chini ya Kocha Hemed Suleiman
Ikiwa mwandalizi mwenza wa michuano ya Afcon 2027 ambayo itafanyika Kenya, Uganda na Tanzania, kufuzu michuano ya mwakani kutatoa nafasi kwa Tanzania kujifunza na kupata uzoefu kabla ya kuandaa michuano hiyo 2027



