Baada ya kutambulishwa na KMC mwishoni mwa juma lililopita, Kally Ongala ameanza rasmi majukumu ya kukinoa kikosi cha KMC
Ongala alitua KMC akichukua mikoba iliyoachwa na Abdihamid Moallin ambaye ametimkia klabu ya Yanga
Kirabua cha kwa kwanza cha Ongala ni mchezo wa ligi kuu dhidi ya Dodoma Jiji ambao utapigwa Novemba 24 katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma
KMC inashika nafasi ya 7 katika msimamo wa ligi kuu ya NBC ikikusanya alama 14 baada ya mechi 11




