Saa 10 jioni timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itakuwa uwanja wa Benjamin Mkapa kusaka tiketi ya fainali ya michuano ya Afcon 2025 dhidi ya Guinea
Ni mchezo ambao Tanzania inahitaji kushinda ili kujihakikishia tiketi ya kushiriki michuano hiyo itakayofanyika Morocco mwakani
Hata hivyo ni wazi haitakuwa kazi rahisi mbele ya Guinea iliyoshinda mechi tatu mfululizo baada ya mara ya mwisho kupoteza mchezo nyumbani kwa kufungwa na Tanzania bao 1-0
Guinea wao wanahitaji alama moja tu kufuzu kwani wako nafasi ya pili kundi H wakiwa na alama 9 huku Tanzania wakiwa wa tatu na alama 7
Ushindi utaifanya Tanzania ifikishe alama 10 na hivyo kuipiku Guinea nafasi ya pili na kuungana na DR Congo kufuzu kwa michuano hiyo
Mchezo huo hautakuwa na kiingilio baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk. Samia Suluhu Hassan kutoa ofa kwa mashabiki kuingia bure dimba la Mkapa ili kuwaongezea hamasa wachezaji
Kila la kheri Tanzania.....!



