Local,Normal News,Pamba, Simba

Simba yaichapa Pamba Jiji 1-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Nov 2024
Simba yaichapa Pamba Jiji 1-0

Simba ameunguruma uwanja wa CCM Kirumba akiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa ligi kuu ya NBC

Simba iliuanza mchezo huo kwa kasi wakipeleka mashambulizi mfululizo katika lango la Pamba Jiji

Mashambulizi hayo yalizaa matunda dakika ya 23 baada ya Lionel Ateba kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari na mwamuzi kuamuru mkwaju wa penati

Alikuwa Ateba aliyeutumbukiza mpira kimiani na kuiandikia Simba bao muhimu ambalo limewahakikishia alama tatu katika mchezo mgumu uliotawaliwa na matumizi ya nguvu

Kipindi cha kipi Pamba Jiji walizinduka lakini haikuwa rahisi kwao kuipenya ngome ya Simba iliyokuwa chini ya mabeki Che Malone Fondoh na Carabou Chamou huku mlinda lango Moussa Camara akifanya kazi ya ziada kuikoa michomo ya washambuliaji wa Pamba Jiji

Ni ushindi ambao unaifanya Simba izidi kujiimarisha kileleni katika msimamo wakifikisha alama 28

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
43m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’