Meneja mpya wa Manchester United Ruben Amorim ameweka kipaumbele cha kumsajili mshambuliaji wa Sweden Viktor Gyokeres kutoka klabu ya zamani ya Sporting msimu ujao lakini Manchester City pia wanamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Sunday Mirror)
Manchester United imefanya mawasiliano na Real Madrid kuhusu uwezekano wa kumsajili kiungo Eduardo Camavinga, 22, lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa hana nia ya kutaka kuondoka. (Bernabeu Digital – In Spanish)
Klabu hiyo ya Old Trafford pia inamfuatilia mlinzi wa pembeni wa Paris St-Germain Mreno Nuno Mendes, 22, ambaye alicheza chini ya Amorim huko Sporting. (Mail on Sunday)
Lakini mabeki watatu walioteuliwa na wamiliki wa Manchester United Ineos ni mchezaji wa kimataifa wa Canada na Bayern Munich Alphonso Davies, 24, Mserbia Milos Kerkez, 21 kutoka Bournemouth na mlinzi wa Benfica Mhispania Alvaro Fernandez Carreras, 21 - ambaye aliondoka Old Trafford msimu uliopita wa joto. (Express)
Aston Villa wamejiunga na klabu kadhaa za Italia kuonyesha nia ya kumnunua mshambuliaji wa Manchester United na Uholanzi Joshua Zirkzee, 23, kwa mkopo mwezi Januari. (Caught Offside) Arsenal wanaweza kutoa ada ya kubwa kumnunua kiungo wa kati wa AC Milan na Uholanzi Tijjani Reijnders, 26, msimu ujao. (Fichajes – In Spanish)
Manchester City wanajitayarisha kumtafuta kiungo wa kati wa Crystal Palace na Uingereza Adam Wharton, 20. (Teamtalk)
Everton wanataka kumsajili winga wa Botafogo na Brazil Luiz Henrique, 23, huku meneja Sean Dyche akijaribu kuboresha safu yake ya ushambuliaji. (Football Insider), Tottenham na Liverpool wameungana na Barcelona katika mbio za kumsajili beki wa pembeni wa Uholanzi Devyne Rensch, 21, kutoka Ajax. (Diario Sport – In Spanish)
Chelsea wamesalia kuwa mashabiki wakubwa wa mshambuliaji wa Brighton na Jamhuri ya Ireland Evan Ferguson, 20, lakini Seagulls watadai pauni milioni 100 kwa mchezaji huyo. (TeamTalks)
Manchester City wanaweza kukatiza mipango ya Chelsea ya kumsajili mshambuliaji wa Ipswich Town Liam Delap, 21, kwa kuwa wana kipengele cha kumnunua tena kwa pauni milioni 20 mchezaji waliyemuuza tu msimu wa joto. (Express)
Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza ya vijana walio chini ya umri wa miaka 21 Lee Carsley ana furaha kukataa nafasi ya usimamizi wa klabu hiyo kwa matumaini ya kurithi mikoba ya Thomas Tuchel kama meneja wa Uingereza mwaka wa 2026. (The Sun)
Beki wa zamani wa Uswidi na Aston Villa Olof Mellberg anatarajiwa kuchukua nafasi ya meneja wa klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya St Louis City. (Goal)
BBC



