Local,Normal News,Simba

Tutafunga kila anayekuja kwa Mkapa - Ahmed

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 Nov 2024
Tutafunga kila anayekuja kwa Mkapa - Ahmed

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema timu hiyo imejipanga kufanya vizuri katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika msimu huu ambapo watahakikisha wanachukua alama tatu katika kila mchezo utakaochezwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Jumatano, Novemba 27 Simba itaikaribisha Bravos ya Angola katika mchezo wa kwanza wa kundi A ambalo linaundwa na timu za Simba, CS Consstantine, CS Sfaxien na Bravos

Akizungumza katika matukio ya kuhamasisha mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa kuishangilia timu yao, Ahmed alisema mkakati wao ni kuvuka hatua ya robo fainali na hivyo ni lazima washinde kila mchezo nyumbani

"Tarehe 27 tuna jambo kubwa kwenye Uwanja wa Mkapa. Tunahitaji kuanza vizuri hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika. Ushindi wa Simba unakutegemea wewe Mwanasimba, tambua ya kwamba tiketi utakayonunua ni silaha muhimu ya kuisaidia Simba siku hiyo"

"Tunatambua siku hiyo ni siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa, ukishamaliza kupiga kura yako elekea Uwanja wa Mkapa. Asibaki Mwanasimba siku hiyo, tambua kwamba ushindi wa Simba unapatikana kwa ushirikiano wa nguvu wa kila Mwanasimba"

"Tumejiandaa siku hiyo kila Mwanasimba atakayekuja uwanjani aondoke na furaha. Tumedhamiria msimu huu kila anayekuja lazima tumefunge. Kwahiyo ndugu zangu Wanasimba jukumu letu la msingi ni kwenda uwanjani na ukienda uwanjani usitulie, unafanya balaa unaloweza," alitamba Ahmed

Aidha Ahmed amejitanga kuwa yeye ndiye atakayekuwa mgeni rasmi katika mchezo huo utakaopigwa Jumatano kuanzia saa 10 jioni

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
59m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’