Licha ya mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) kati ya Simba dhidi ya Bravos do Maquis kupigwa hapo kesho, timu hiyo kutoka Angola bado haijawasili nchini
Bravos do Maquis wameficha taarifa za ujio wao lakini huenda wakatua leo mchana
Timu hiyo ilipaswa kufanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa Benjamin Mkapa leo asubuhi kwa kuwa jioni kutakuwa na mchezo kati ya Yanga dhidi ya Al Hilal
Imeelezwa Bravos do Maquis wameamua kukamilisha maandalizi yao huko kwao, kabla ya kuja nchini
Upande wa wenyeji Simba wanaendelea na maandalizi kuelekea mchezo huo ambapo leo Simba itakamilisha maandalizi yake tayari kwa mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni



