Wapinzani wa Simba CAF CC bado hawajafika

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th November 2024


Wapinzani wa Simba CAF CC bado hawajafika

Licha ya mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) kati ya Simba dhidi ya Bravos do Maquis kupigwa hapo kesho, timu hiyo kutoka Angola bado haijawasili nchini

Bravos do Maquis wameficha taarifa za ujio wao lakini huenda wakatua leo mchana

Timu hiyo ilipaswa kufanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa Benjamin Mkapa leo asubuhi kwa kuwa jioni kutakuwa na mchezo kati ya Yanga dhidi ya Al Hilal

Imeelezwa Bravos do Maquis wameamua kukamilisha maandalizi yao huko kwao, kabla ya kuja nchini

Upande wa wenyeji Simba wanaendelea na maandalizi kuelekea mchezo huo ambapo leo Simba itakamilisha maandalizi yake tayari kwa mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.