Local,Normal News,Simba, Bravos

Simba yaanza vyema CAF CC, yaichapa Bravos Fc 1-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Nov 2024
Simba yaanza vyema CAF CC, yaichapa Bravos Fc 1-0

Simba imeanza vyema kampeni ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika hatua ya makundi ikipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Bravos Fc ya Angola katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Jean Charles Ahoua ameendeleza moto wake wa kuzifumania nyavu leo tena akifunga bao pekee la ushindi kupitia mkwaju wa mapema katika kipindi cha kwanza baada ya beki wa Bravos kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari

Simba ilitawala mchezo katika kipindi cha kwanza ikitengeneza nafasi kadhaa lakini umakini ulikosekana kwa washambuliaji Steven Mukwala, Kibu Denis na Ahoua wakishindwa kutumia nafasi hizo

Kipindi cha pili Bravos walirejea wakiwa imara na wangesawazisha bao hilo kama sio umahiri wa mlinda lango wa Simba Moussa Camara aliokoa mkwaju wa penati

Ni aina ya mechi ambayo mashabiki wa Simba watafurahia alama tatu lakini ni wazi kocha Fadlu Davids atahitaji kuendelea kukiboresha kikosi chake ili kuhakikisha malengo ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo yanafikiwa

More Stories

Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
9h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE β†’
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
1d ago
READ MORE β†’