International,Transfer News,

Tetesi za usajili Jumamosi, Novemba 30 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Nov 2024
Tetesi za usajili Jumamosi, Novemba 30 2024

Real Madrid wameifahamisha Liverpool kuhusu nia yao ya kutaka kumsajili beki wa Uingereza Trent Alexander-Arnold, 26. (TalkSport)

Kocha mpya wa Manchester United Ruben Amorim ameazimia kufanya kazi na wachezaji wake wa sasa na hajatuma ombi kwa uongozi wa klabu kuhusu usajili wowote wa Januari. (Sky Sports)

Tottenham wana nia ya kumsajili beki wa kulia wa RB Leipzig Mholanzi Lutsharel Geertruida, mweney umri wa miaka 24, kama kiungo mbadala wa Pedro Porro, mwenye umri wa miaka 25, ambaye analengwa na Real Madrid . (Caught Offside)

Mshambuliaji wa Ipswich Town mwenye umri wa miaka 21, Liam Delap anavutiwa na vilabu kadhaa vya Ligi ya Primia. (Athletic - subscription required)

Manchester United na Tottenham zinaendelea kuhusishwa na taarifa za kutaka kumnunua Cunha lakini meneja wa Wolves Gary O'Neil amekataa kuondoka Januari. (MEN)

Aston Villa wanakaribia kufikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa kati wa Werner Bremen na Austria Romano Schmid, mwenye umri wa miaka 24. (Football Insider)

Chelsea wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Denmark Patrick Dorgu, 20, kutoka Lecce , ambaye anaweza kuhitaji malipo ya takriban £50m. (Caught Offside)

Wolves itampatia kandarasi mpya yenye faida kubwa mshambuliaji wa Brazil ambaye yuko katika hali nzuri kimchezo Matheus Cunha, ambaye ana umri wa miaka 25 (Telegraph - subscription required)

Everton wanataka kuendelea kuwa na mshambuliaji wa Uingereza Dominic Calvert-Lewin, mwenye umri wa miaka 27, Januari licha ya uvumi kuhusu mustakabali wake. (Football Insider)

Tottenham, Crystal Palace na Nottingham Forest pia wanavutiwa na Dorgu. (TBR)

Hatua ya Arsenal ya kutaka mshambuliaji mpya imepata pigo kwa Viktor Gyokeres, 26, anayetaka kumfuata meneja wa zamani wa Sporting Lisbon Ruben Amorim kwenda Manchester United. (Football.London)

Beki wa Crystal Palace, 24, Muingereza, Marc Guehi, anatamani kujiunga tena na Chelsea, wakati Newcastle pia bado wanavutiwa na beki huyo wa kati. (TeamTalk)

Manchester City na Manchester United wamepewa fursa ya kumnunua kiungo wa kati wa Brazil Douglas Luiz, 26, na kiungo wa kati wa Italia na Juventus Fagioli, 23, . (Gazzetta dello Sport - In Itali)

Meneja wa Chelsea Enzo Maresca amekanusha kuwa Christopher Nkunku anauzwa, licha ya fowadi huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 27 kuwa na muda mfupi wa kucheza. (Times - Subnscription Required)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’