Yanga yaichapa Namungo Fc 2-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th November 2024


Yanga yaichapa Namungo Fc 2-0

Yanga imezoa alama zote tatu mkoani Lindi wakiichapa Namungo Fc mabao 2-0 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Majaliwa, Ruangwa

Mabao ya kipindi cha pili yaliyofungwa na Kennedy Musonda na Pacome Zouzoua, yalitosha kuihakikishia Yanga alama tatu muhimu 

Vijana wa Kocha Sead Ramovic waliingia katika mchezo huo wakiwa na ari ya kusaka ushindi, ilikuwa ni suala la muda tu Yanga kufunga baada ya kwenda mapumziko matokeo yakiwa suluhu ya bila kufungana

Namungo walishindwa kuhimili kasi ya Yanga katika kipindi cha pili, Kennedy Musonda akifunga bao la kwanza dakika ya 50 akimalizia pasi ya Maxi Nzengeli kabla ya Pacome kufunga la pili dakika ya 67 akimalizia pasi ya Clatous Chama aliyeingia kuchukua nafasi ya Aziz Ki

Ni ushindi wa kwanza kwa Ramovic huku Namungo Fc ikiendelea kuchechemea ikipoteza mechi ya tatu mfululizo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.