Yanga imezoa alama zote tatu mkoani Lindi wakiichapa Namungo Fc mabao 2-0 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Majaliwa, Ruangwa
Mabao ya kipindi cha pili yaliyofungwa na Kennedy Musonda na Pacome Zouzoua, yalitosha kuihakikishia Yanga alama tatu muhimu
Vijana wa Kocha Sead Ramovic waliingia katika mchezo huo wakiwa na ari ya kusaka ushindi, ilikuwa ni suala la muda tu Yanga kufunga baada ya kwenda mapumziko matokeo yakiwa suluhu ya bila kufungana
Namungo walishindwa kuhimili kasi ya Yanga katika kipindi cha pili, Kennedy Musonda akifunga bao la kwanza dakika ya 50 akimalizia pasi ya Maxi Nzengeli kabla ya Pacome kufunga la pili dakika ya 67 akimalizia pasi ya Clatous Chama aliyeingia kuchukua nafasi ya Aziz Ki
Ni ushindi wa kwanza kwa Ramovic huku Namungo Fc ikiendelea kuchechemea ikipoteza mechi ya tatu mfululizo



