Azam Fc kuongoza ligi leo?

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st December 2024


Azam Fc kuongoza ligi leo?

Azam Fc inaweza kupanda kileleni mwa msimamo wa ligi leo kama itaibuka na ushindi dhidi ya Dodoma Jiji katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma

Azam Fc wana alama 27 katika nafasi ya pili huku Simba inayoongoza ligi ikiwa na alama 28

Kama Azam Fc itashinda mchezo huo ugenini, itafikisha alama 31 na kuiondoa Simba kileleni

Mtanange huo unatarajiwa kupigwa kuanzia saa 3 usiku. Kutakuwa na mechi nyingine mbili ambazo zitapigwa mapema leo

Pamba Jiji watakuwa wenyeji wa KenGold uwanja wa CCM Kirumba huku Coastal Union wakiikabiri Prisons huko Arusha


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.