Mshambuliaji wa Manchester City Erling Haaland amewaka mashabiki wa wachezaji wenzake wa timu hiyo kuwa na imani licha ya hali yao mbaya
Mabingwa hao wa Premier League hawajashinda katika mechi saba katika michuano yote kwa mara ya kwanza tangu 2004
Man City pia wako kwenye mwenendo mbaya zaidi wa ligi tangu 2008. Kichapo cha Jumapili dhidi ya Liverpool kilikuwa cha nne mfululizo kwa City, sawa na rekodi kama hiyo ya miaka 16 iliyopita
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X, Haaland aliandika ujumbe akiwataka wafuasi wa timu hiyo wawe na utulivu
"Tumeona bora siku zilizopita, na tutaona tena. Tuendelea kuamini," alindika Haaland
City waliteremka hadi nafasi ya tano kwenye jedwali baada ya kichapo huko Merseyside na sasa wameachwa alama 11 na vinara Liverpool
Watakuwa na matumaini ya kupunguza pengo lao nyumbani kwa Nottingham Forest Jumatano