Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Disemba 04 2024

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th December 2024


Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Disemba 04 2024

Nottingham Forest inajiandaa kuwasilisha dau la kumnunua mshambuliaji wa Brighton na Jamhuri ya Ireland Evan Ferguson, 20, mwezi Januari . (Football Insider)

Real Madrid wanataka kumsajili beki wa Liverpool kutoka Uingereza Trent Alexander-Arnold, 26, kwa uhamisho wa bure. (Telegraph - usajili unahitajika)

Liverpool wanapanga kufanya uhamisho wa pauni milioni 91 Januari kwa beki wa Bournemouth mwenye umri wa miaka 21 na Hungary Milos Kerkez na kiungo wa Real Sociedad na Uhispania Martin Zubimendi, 25. (Teamtalk)

Arsenal, Chelsea, Liverpool na Tottenham ni miongoni mwa vilabu vinavyomuwania winga wa Athletic Bilbao mwenye umri wa miaka 22 Nico Williams. (Athletic -Usajili unahitajika)

Barcelona wanamfuatilia mshambuliaji wa Newcastle United na Uswidi Alexander Isak, 25. (Caught Offside)

Manchester United wana nia ya kumsajili beki wa RB Leipzig wa Ujerumani David Raum, 26, na mshambuliaji wa Juventus na Uturuki Kenan Yildiz, 19. (Sky Germany - kwa Kijerumani)

Manchester United wamewasiliana na beki wa Canada Alphonso Davies, 24, ili kutathini nia yake ya kujiunga na klabu hiyo mkataba wake wa Bayern Munich utakapokamilika msimu ujao. (Team Talk)

Leicester City wana nia ya kuimarisha safu yao ya mashambulizi na wana mpango wa kumsajili mshambuliaji mpya dirisha la uhamisho wa wachezaji litakapofunguliwa Januari. (Football Insider)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.