Local,Normal News,Yanga, Alger

MC Alger vs Yanga kupigwa bila mashabiki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Dec 2024
MC Alger vs Yanga kupigwa bila mashabiki

Leo Yanga inatarajiwa kutua Algiers yalipo Makao Makuu ya Algeria tayari kwa mchezo wa pili wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya MC Alger

Mchezo huo utapigwa Jumamosi, Disemba 07 katika uwanja wa Julai 05, 1962 saa 1 usiku

Yanga inarudi katika uwanja huu mwaka mmoja baada ya mchezo wao wa fainali ya kombe la Shirikisho dhidi ya USM Alger uliomlizika kwa Wananchi kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa Djuma Shaban dakika ya 7 baada ya Kennedy Musonda kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari

Ni hapa hapa Yanga ilicheza mechi ngumu sana iliyogubikwa na kila aina ya matukio ya kustaajabisha katika soka kwani yalipigwa hadi mabomu ya machozi!

Wakati huu wanarudi kucheza dhidi ya MC Alger timu yenye upinzani wa jadi na USM Alger katika mchezo mwingine ambao Yanga inahitaji kushinda

Lakini wakati huu mambo yatakuwa tofauti kwani zile vurugu ambazo Yanga walifanyiwa mwaka jana hazitarajiwi kuwepo

Klabu ya MC Alger imefungiwa kuingiza mashabiki katika mechi zao mbili za nyumbani kufuatia vurugu za mashabiki wao katika mchezo wa kuwania kutinga hatua ya makundi CAF CL dhidi ya US Monastir

Yanga itakuwa timu ya kwanza kucheza na MC Alger bila mashabiki ikiwa sehemu ya kutekeleza kifungo hicho

MC Alger walikata rufaa lakini CAF ilishikilia msimamo huku pia wakigomea maombi ya klabu hiyo kubadili uwanja

Bila shaka kocha Sead Ramovic na vijana wake watakuwa na nafasi ya kufanya vizuri katika mchezo huu ambao hautakuwa na presha kutoka kwa mashabiki

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
59m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’