International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Disemba 05 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
5 Dec 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Disemba 05 2024

Arsenal wamefanya mazungumzo ya awali na mshambuliaji wa Wolves wa Brazil Matheus Cunha, 25. (Caught Offside)

Beki wa Uholanzi Virgil van Dijk amepokea ofa ya mkataba kutoka kwa Liverpool lakini haiendani na matarajio ya mchezaji huyo wa miaka 33. (Athletic - usajili unahitajika)

Mustakabali wa Julen Lopetegui kama kocha mkuu wa West Ham uko kwenye mizani. (Sky Sports)

Edin Terzic, Roger Schmidt, Sergio Conceicao na Massimiliano Allegri ni miongoni mwa wakufunzi wanaowaniwa na West Ham. (Telegraph - usajili unahitajika)

West Ham pia inavutiwa na kocha wa zamani wa Brighton na Chelsea Graham Potter. (Times - usajili unahitajika)

Rodri ameiomba Manchester City kumnunua mchezaji mwenza wa kimataifa na winga wa Athletic Bilbao Nico Williams, 22. (Metro)

Beki wa Uingereza Harry Maguire, 31, anawaniwa klabu kadhaa za Ligi Kuu ya England huku mushtakabili wake katika klabu ya Manchester United ukiwa haujulikani. (Football Insider)

Kocha wa Paris St-Germain Luis Enrique hataki klabu hiyo ya Ufaransa kumleta mshambuliaji wa Sporting na Sweden Viktor Gyokeres, 26, ambaye amekuwa akihusishwa na Manchester City na Manchester United. (Foot Mercato)

Newcastle United inawafuatilia winga wa Bournemouth na Ghana Antoine Semenyo, 24, na mshambuliaji wa Brentford wa Cameroon Bryan Mbuemo, 25. (The i News - usajili unahitajika)

Arsenal na Liverpool wanamfuatilia winga wa LA Galaxy mwenye umri wa miaka 23 kutoka Brazil Gabriel Pec. (Caught Offside)

Hull City wanatazamia kumteua mkufunzi wa Reading Ruben Selles kama kocha wao mpya, huku Alex Neil na Slavisa Jokanovic wakiwa miongoni mwa wengine wanaowania nafasi hiyo. (Telegraph - usajili unahitajika)

Klabu za EPL zinamfuatilia mshambuliaji wa Celtic wa miaka 18 Daniel Cummings. (Mail- usajili unahitajika)

Crystal Palace wanatazamiwa kumsajili mshambuliaji wa Australia Rylan Brownlie mwenye umri wa miaka 17 kwa uhamisho wa bure. (Football Insider)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’