Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba Ahmed Ally amesema kuwa matokeo waliyopata dhidi ya CS Constantine ni mabaya kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuwa walifanya makosa ndani ya dakika tano ambayo yaliwagharimu
Kwenye mchezo uliochezwa Desemba 8 2024 Simba walitangulia kufunga dakika ya 24 kupitia kwa Zimbwe na walifungwa mabao mawili kipindi cha pili dakika ya 47 kwa beki Hamza kujifunga na dakika ya 51 kupitia kwa nahodha wa CS Constantine, Jian
Ahmed amesema baada ya mchezo huo wanarejea nyumbani Tanzania kwa ajili ya mchezo unaofuata dhidi ya CS Sfaxien utakaopigwa Disemba 15 uwanja wa Benjamin Mkapa
"Matokeo tuliyopata dhidi ya CS Constantine ni mabaya na kilichotokea hatuwezi kubadili sasa ni hesabu kuelekea mchezo wetu wa tarehe 15 ambapo tutakuwa nyumbani kwenye mchezo wa hatua ya makundi"
"Kikubwa kuelekea kwenye mchezo wetu mashabiki tuungane kwenye kampeni za kusaka ushindi kwani matokeo yaliyopita tukiwa nyumbani tulipata pointi tatu na sasa ni kuelekea mchezo wetu wa pili tukiwa nyumbani, Uwanja wa Mkapa," alisema Ahmed
Mchezo unaofuata Simba inachuana na CS Sfaxine iliyotoka kupoteza kwa kufungwa mbaoa 3-2 dhidi ya Bravos wote wakiwa kundi A ambalo vinara ni CS Constantine yenye pointi sita



