Local,Normal News,Yanga, Mazembe

Yanga kuifuata TP Mazembe Alhamisi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 Dec 2024
Yanga kuifuata TP Mazembe Alhamisi

Baada ya kurejea kutoka Algeria jana, kikosi cha Yanga Alhamisi kinatarajiwa kuondoka jijini Dar es salaam kuelekea Lubumbashi DR Congo kwa ajili ya mchezo wa raundi ya tatu ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe

Jumamosi, Disemba 14 2024 TP Mazembe watakuwa wenyeji wa Yanga katika mchezo muhimu wa kundi A

Yanga imepoteza mechi zote mbili zilizopita, haipaswi kupoteza mchezo huo ili kufufua matumaini ya kufuzu robo fainali

Utakuwa mchezo mgumu kwani hata TP Mazembe ni mechi ambayo watahitaji kushinda ili kuwa na nafasi ya kufuzu robo fainali

Mazembe wanashika nafasi ya tatu kundi A wakiwa na alama moja ambayo waliipata kwa kulazimishwa suluhu ya bila kufungana na MC Alger hapo Lubumbashi

Mechi dhidi ya Yanga itakuwa mechi yao ya pili nyumbani na pengine inaweza kuamua hatma yao katika ligi ya mabingwa msimu huu

Hivyo Wananchi watakwenda Lubumbashi huku wakifahamu wanakwenda kucheza mechi ya 'jasho na damu'

Lakini Yanga ina kumbukumbu nzuri katika dimba la Mazembe kwani mara ya mwisho walipocheza katika uwanja huo msimu wa 2022/23 katika kombe la Shirikisho, Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’