Kuelekea dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa Jumatatu, Disemba 16, klabu ya Pamba Jiji imetambulisha usajili wak wa kwanza Deus Kaseke
Kaseke ametua Pamba Jiji akiwa mchezaji huru klabu yake ya mwisho kuitumikia ikiwa ni Fountain Gate
Kiungo mkongwe huyo pia amewahi kuzitumikia Mbeya City, Singida United na Yanga ambayo ndio klabu aliyoitumikia kwa muda mrefu zaidi
"Jina lake sio geni masikioni na machoni mwa wanamichezo labda wageni wa mpira wa miguu. Uwezo na uzoefu wake wakucheza nafasi nyingi kiwanjani (Versatile player) imetufanya tumuongeze kwenye safari yetu ya matumaini na kuiletea heshima Timu yetu #TPLINDANDA"
"Kacheza timu nyingi hapa nchini ila kutovaa jezi ya Tp Lindanda kunakitu kingepunguwa," sehemu ya taarifa ya Pamba Jiji ilisomeka



