Pamba Jiji yaanza na Kaseke

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th December 2024


Pamba Jiji yaanza na Kaseke

Kuelekea dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa Jumatatu, Disemba 16, klabu ya Pamba Jiji imetambulisha usajili wak wa kwanza Deus Kaseke

Kaseke ametua Pamba Jiji akiwa mchezaji huru klabu yake ya mwisho kuitumikia ikiwa ni Fountain Gate

Kiungo mkongwe huyo pia amewahi kuzitumikia Mbeya City, Singida United na Yanga ambayo ndio klabu aliyoitumikia kwa muda mrefu zaidi

"Jina lake sio geni masikioni na machoni mwa wanamichezo labda wageni wa mpira wa miguu. Uwezo na uzoefu wake wakucheza nafasi nyingi kiwanjani (Versatile player) imetufanya tumuongeze kwenye safari yetu ya matumaini na kuiletea heshima Timu yetu #TPLINDANDA"

"Kacheza timu nyingi hapa nchini ila kutovaa jezi ya Tp Lindanda kunakitu kingepunguwa," sehemu ya taarifa ya Pamba Jiji ilisomeka


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.