Local,Normal News,Yanga, Mazembe

Kocha Yanga matumaini kibao Congo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Dec 2024
Kocha Yanga matumaini kibao Congo

Kocha Mkuu wa Yanga Sead Ramovic amewashukuru mashabiki wa timu hiyo waliosafiri kwa basi kutoka Tanzania hadi Lubumbashi DR Congo kuishangilia timu yao kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa kesho

Akizungumza na wanahabari kuelekea mchezo huo, Ramovic amesema ujio wa mashabiki hao umewaongezea hamasa wachezaji wake ambao anaamini kesho watapambana ili kuhakikisha wanawapa furaha

"Ni jambo kubwa sana ambalo Mashabiki wa Yanga wamelifanya, kusafiri kwa Basi kutoka Dar Es Salaam mpaka hapa Lubumbashi siyo rahisi"

"Ni faraja kwetu na inatupa motisha ya kuwa tuna watu wanaotupa moyo na kutufanya tusiyumbe, kwakweli nachoweza kusema ni kwamba tupo hapa kwaajili ya kuwapa furaha, timu nzima inatambua umuhimu wa mashabiki wetu, panapo majaaliwa kesho tutapambana kuhakikisha tunawafurahisha Wananchi," alisema Ramovic

Akizungumzia maandalizi ya kikosi chake, Ramovic amesema wamejiandaa kufanya vizuri katika mchezo huo ambao anatarajia utakuwa mgumu

"Malengo yetu ni kuonesha uwezo wetu na kufanya vizuri kesho, Haijalishi wapinzani wetu wakoje. Sisi tunafahamu TP Mazembe ni timu kubwa na ina Wachezaji wazuri hivyo kesho tutashuhudia mechi nzuri sana"

"Nafahamu kuwa mchezo wa mwisho hapa Congo Yanga ilishinda lakini hatuwezi kuzungumzia yaliyopita, tunautazama mchezo wa kesho kama mchezo mpya na tupo tayari kwa changamoto hii," alisema

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, kiungo Maxi Nzengeli amesema wachezaji wako tayari kuonyesha ubora wao katika mchezo wa kesho na lengo ni kushinda

"Tunamshukuru Mungu tumefika salama, tupo hapa Lubumbashi kwaajili ya kupambana, ni kweli hatujashinda mechi zetu za mwanzo lakini haimaanishi tukae vichwa chini, huu ni muda wa kurudi juu na kuwapa furaha wananchi, tunatambua ukubwa wa Mazembe lakini tutapambana kwaajili ya kushinda kesho"

"Tunasema asante kwa mashabiki wa Yanga siyo rahisi kusafiri kwa basi mpaka hapa, haitakuwa rahisi lakini tunawahakikishia tutapambana sana kwaajili yao, Tunashukuru sana kwa kujitoa kwa ajili ya timu," alisema Maxi

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
59m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’