Alama moja muhimu imepatikana Lubumbashi baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya TP Mazembe katika mchezo wa raundi ya tatu hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika
Bao la dakika za lala salama lililofungwa na Prince Dube limeihakikishia Yanga kuondoka na alama moja Congo katika mchezo ambao pengine Yanga ingeweza kuibuka na ushindi kama umakini katika eneo la mbele ungekuwa mkubwa
Baada ya kufunga bao katika kipindi cha kwanza Mazembe walitumia muda mwingi kuzuia lakini haikutosha kwao kuondoka na uashindi nyumbani
Yanga ina mechi nyingine tatu za kufuzu robo fainali mbili zikiwa nyumbani dhidi ya Mazembe na MC Alger
Mwanzoni mwa Januari 2025 Mazembe itasafiri Tanzania kumenyana na Yanga