Singida BS vs Simba kupigwa Disemba 28

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th December 2024


Singida BS vs Simba kupigwa Disemba 28

Bodi ya Ligi Kuu imefanya maboresho ya ratiba ya michezo miwili ya Simba

Mchezo dhidi ya Singida Big Stars ambao awali haukupangiwa tarehe sasa utachezwa Disemba 28, 2024 kwenye Uwanja wa Liti mkoani Singida

Mchezo dhidi ya Tabora United ambao ulipangwa kuchezwa Disemba 28, 2024 kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora umeondolewa na utapangiwa tarehe mpya

Maboresho hayo pia yamegusa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Fountain Gate ambao sasa umepangwa kupigwa DIsemba 29 na kuondolewa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Kagera Sugar ambao awali ulipangwa kupigwa Disemba 29

Haya hapa maboresho kamili ya ratiba


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.