Bodi ya Ligi Kuu imefanya maboresho ya ratiba ya michezo miwili ya Simba
Mchezo dhidi ya Singida Big Stars ambao awali haukupangiwa tarehe sasa utachezwa Disemba 28, 2024 kwenye Uwanja wa Liti mkoani Singida
Mchezo dhidi ya Tabora United ambao ulipangwa kuchezwa Disemba 28, 2024 kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora umeondolewa na utapangiwa tarehe mpya
Maboresho hayo pia yamegusa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Fountain Gate ambao sasa umepangwa kupigwa DIsemba 29 na kuondolewa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Kagera Sugar ambao awali ulipangwa kupigwa Disemba 29
Haya hapa maboresho kamili ya ratiba




