Fei Toto afikia rekodi yake ya msimu uliopita

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th December 2024


Fei Toto afikia rekodi yake ya msimu uliopita

Azam Fc jana iliendeleza dhamira yake ya kuwania ubingwa wa ligi kuu msimu huu wakiichapa Fountain Gate mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa dimba la Azam Complex

Ilikuwa siku nyingine ya kuzishuhudia 'shoo' za kiungo mahiri wa timu Feisal Salum 'Fei Toto' ambaye jana aliongeza assist yake ya 7 msimu huu na kufikia rekodi aliyoweka msimu uliopita

Katika msimu wa 2023/24 Fei Toto alitumia mechi 30 kufunga mabao 19 na kutoa assist 7, mpaka sasa msimu huu amepachika mabao 3 na kutoa assist 7 ndani ya mechi 15 akiwa amehusika katika mabao 10

Kilichopungua msimu huu kutoka kwake ni idadi ya mabao ya kufunga na pengine hilo linatokana na mabadiliko ya benchi la ufundi ambayo yamepelekea kiungo huyo kupewa majukumu tofauti ya kuchezesha na kutengeneza nafasi zaidi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.