Simba imeendeleza ubabe wake katika ligi kuu ya NBC ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya KenGold katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC Complex
Mabao ya kipindi cha kwanza yaliyowekwa kambani na mshambuliaji Lionel Ateba yalitosha kuihakikishia Simba alama tatu muhimu katika mchezo ambao pengine Mnyama angeweza kuondoka na ushindi mnono zaidi
Bao la kwa Ateba alifunga kupitia mkwaju wa penati dakika ya 35 baada ya Awesu Awesu kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari kisha kuongeza la pili dakika chache baadae kwa mpira wa kichwa akimaliza mpira wa kona kutoka kwa Valentine Nouma
Kipindi cha pili Simba iliendelea kutawala mchezo lakini mpaka dakika 90 zinamalizika ubao ulisoma 2-0
Ni ushindi ambao unairejesha Simba katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 31