Mwenyekiti Kamati ya uchaguzi Dar afungiwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th December 2024


Mwenyekiti Kamati ya uchaguzi Dar afungiwa

Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemfungia miaka mitano kujihusisha na mpira wa miguu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salam (DRFA), Yusuph Kaiwanga

Katika uamuzi wake, Kamati imesema baada ya kupitia ushahidi wa nyaraka na maelezo ya shahidi imejiridhisha pasi na shaka kuwa Mlalamikiwa Kaiwanga alitenda makosa kwa makusudi

Kamati ilijiridhisha kuwa Mlalamikiwa hakutumia vyema mamlaka aliyopewa kisheria kusimamia uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Temeke (TEFA) na kuamua kuufuta

Hatua yake ya kuufuta haikuwa sahihi kwa vile alishiriki mchakato mzima wa uchaguzi huo

Hivyo, Kamati ya Maadili imeamua matokeo ya uchaguzi wa TEFA yanabaki kama yalivyo

Mbali ya kifungo cha miaka mitano, Kamati pia imemtoza mlalamikiwa faini ya sh. milioni sita

Adhabu hizo zimetolewa chini ya kifungu cha 73(4) na (5) cha Kanuni za Maadili za TFF, Toleo la 2021

Awali Kaiwanga alilalamikiwa mbele Kamati ya Maadili kuwa kitendo chake cha kufuta Uchaguzi wa TEFA wakati alishiriki mchakato mzima tangu mwanzo kilikiuka Kanuni za Maadili za TFF.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.