Yanga imeanza vyema matumizi ya uwanja wa KMC Complex wakiibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mashujaa Fc
Ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Yanga kutumia uwanja wa KMC Complex na wameandikisha alama tatu za kwanza
Alikuwa ni Prince Dube aliyepeleka furaha Jangwani akifunga mabao yote matatu na kuondoka na mpira
Ni hat-trik ya kwanza kufungwa msimu huu na kwa Wananchi ni furaha zaidi kwa Dube kuwa mfungaji wa hat-trik hiyo
Dube hakuanza vyema msimu lakini mabao yake matatu leo yatamuongezea kujiamini na kufufua matumaini katika mbio za ufungaji bora
Haikuwa siku nzuri kwa mlinda lango Aboubakar Khomein ambaye aliruhusu kufungwa mabao mawili ya mashuti ya mbali yaliyopigwa na David Ulomi na Idris Stambuli
Ni ushindi muhimu kwa Yanga ambao unawafanya wafikishe alama 30 katika nafasi ya tatu



