Dube apiga hat-trik Yanga ikiichapa Mashujaa Fc 3-2

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th December 2024


Dube apiga hat-trik Yanga ikiichapa Mashujaa Fc 3-2

Yanga imeanza vyema matumizi ya uwanja wa KMC Complex wakiibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mashujaa Fc

Ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Yanga kutumia uwanja wa KMC Complex na wameandikisha alama tatu za kwanza

Alikuwa ni Prince Dube aliyepeleka furaha Jangwani akifunga mabao yote matatu na kuondoka na mpira

Ni hat-trik ya kwanza kufungwa msimu huu na kwa Wananchi ni furaha zaidi kwa Dube kuwa mfungaji wa hat-trik hiyo

Dube hakuanza vyema msimu lakini mabao yake matatu leo yatamuongezea kujiamini na kufufua matumaini katika mbio za ufungaji bora

Haikuwa siku nzuri kwa mlinda lango Aboubakar Khomein ambaye aliruhusu kufungwa mabao mawili ya mashuti ya mbali yaliyopigwa na David Ulomi na Idris Stambuli

Ni ushindi muhimu kwa Yanga ambao unawafanya wafikishe alama 30 katika nafasi ya tatu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.