Yanga imerejesha 5G katika ligi kuu ya NBC leo wakiichabanga Fountain Gate mabao 5-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC Complex
Yanga ilitawala mchezo huo tangu mwanzo wa kipindi cha kwanza lilikuwa ni suala la muda kwa Yanga kuanza kuhesabu mabao kutokana na mashambulizi mfululizo waliyopeleka langoni kwa Fountain Gate
Alikuwa ni Pacome Zouzoua aliyefunga kalamu ya mabao akiunganisha krosi ya Chadrack Boka kutoka upande wa kushoto
Yanga ikaongeza mabao mengine mawili kabla ya mapumziko kupitia kwa Mudathir Yahya na Pacome kwa mara nyingine
Pacome almanusra aondoke na hat-trik shuti lake la mapema kipindi cha pili likiguswa na mlinda lango wa Fountain Gate John Noble kabla Shiga kumalizia mpira uliogonga mwamba
Clement Mzize ndiye aliyekamilisha kipigo kwa Fountain Gate akimalizia mpira kutoka kwa Salum Abubakar 'Sure Boy'
Ni ushindi wa tano mfululizo kwa kocha Sead Ramovic Yanga ikikusanya alama 15 chini yake na kufunga mabao 18
Yanga sasa ndio timu iliyofunga mabao mengi zaidi msimu huu