Ahoua aendelea kudhihirisha umahiri wake Msimbazi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th January 2025


Ahoua aendelea kudhihirisha umahiri wake Msimbazi

Jana kiungo mshambuliaji wa Simba Jean Charles Ahoua alifunga bao lake la pili katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika nchini Tunisia

Katika mabao matano yaliyofungwa na Simba kwenye hatua ya makundi, Ahoua amehusika mabao matatu

Alifunga katika mchezo dhidi ya Bravos na kutoa pasi ya bao katika mchezo wa kwanza dhidi ya CS Sfaxien

Licha ya kocha mkuu wa Simba Fadlu Davids kusema nyota huyo hajafikia asilimia 100 ya uwezo wake, Fadlu ameendele kutengeneza takwimu za kutisha tangu alipotua Simba

Katika ligi kuu, amehusika kwenye mabao 12 akifunga 7 na kutoa pasi tano za mabao

Jumla Ahoua amehusika katika mabao 15 yliyofungwa na Simba msimu huu katika mashindano yote

katika msimu wake wa kwanza ndani ya Simba, umri wake ukiwa ni miaka 22, takwimu hizi zinadhihirisha kipaji alichonacho kiungo huyo raia wa Ivory Coast


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.