Jana kiungo mshambuliaji wa Simba Jean Charles Ahoua alifunga bao lake la pili katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika nchini Tunisia
Katika mabao matano yaliyofungwa na Simba kwenye hatua ya makundi, Ahoua amehusika mabao matatu
Alifunga katika mchezo dhidi ya Bravos na kutoa pasi ya bao katika mchezo wa kwanza dhidi ya CS Sfaxien
Licha ya kocha mkuu wa Simba Fadlu Davids kusema nyota huyo hajafikia asilimia 100 ya uwezo wake, Fadlu ameendele kutengeneza takwimu za kutisha tangu alipotua Simba
Katika ligi kuu, amehusika kwenye mabao 12 akifunga 7 na kutoa pasi tano za mabao
Jumla Ahoua amehusika katika mabao 15 yliyofungwa na Simba msimu huu katika mashindano yote
katika msimu wake wa kwanza ndani ya Simba, umri wake ukiwa ni miaka 22, takwimu hizi zinadhihirisha kipaji alichonacho kiungo huyo raia wa Ivory Coast



