International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Januari 11 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Jan 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Januari 11 2025

Aston Villa wameongeza dau la kumnunua mshambuliaji wa Borussia Dortmund Donyell Malen hadi euro milioni 25 (£21m), lakini timu hiyo ya Ujerumani bado inadai euro milioni 30 (£25.1m) kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi, 25. (Florian Plettenberg)

Manchester United, Arsenal na Liverpool zinamtaka kiungo wa kati wa Wolves na Brazil mwenye umri wa miaka 23 Joao Gomes. (Sun)

Monaco ni klabu ya hivi karibuni kuonesha nia ya kumsajili mshambuliaji wa Manchester United mwenye umri wa miaka 27 raia wa England Marcus Rashford. (Telegraph)

Paris St-Germain wanamtaka mshambuliaji wa Aston Villa mwenye umri wa miaka 21 raia wa Colombia Jhon Duran. (RMC Sport)

Manchester United wanafanya kila wawezalo kuipiku Tottenham katika usajili wa mshambuliaji wa Paris St-Germain raia wa Ufaransa Randal Kolo Muani mwenye umri wa miaka 26. (Team Talk)

Brighton na Borussia Dortmund wanavutiwa na winga wa Liverpool mwenye umri wa miaka 21 Harvey Elliott. (Sun )

Ipswich inachunguza mpango wa kumsajili kiungo wa zamani wa Serbia Nemanja Matic, 36, kutoka Lyon. (Florian Plettenberg)

Kiungo wa kati wa Bournemouth na Denmark Philip Billing amesafiri kwa ndege hadi Italia kukamilisha uhamisho wa mkopo kwenda Napoli. (Fabrizio Romano)

Everton wanafikiria kuwasilisha ombi la kumnunua winga wa Lyon wa Ghana Ernest Nuamah, 21. (RMC Sport )

Leicester wamekubali dili la kumsaini beki wa pembeni wa Ufaransa Woyo Coulibaly, 25, kutoka Parma. (Gianluca di Marzio)

Fenerbahce wamefanya mazungumzo na Aston Villa kuhusu mkataba wa £10m kwa beki wao wa kati Mbrazil Diego Carlos, 31. (Sky Sports)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’