Timu ya Taifa ya Zanzibar 'Zanzibar Heroes' jana ilifanikiwa kulibakisha kombe la Mapinduzi nyumbani baada ya kuichapa Burkina Faso mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa Gombani, Pemba
Bao la dakika za lala salama lililofungwa na Hassan Ali Cheda lilitosha kuihakikisha Heroes ushindi huo muhimu katika mchezo wa kuadhimisha kilele cha sherehe za kumbukumbu ya Mapinduzi Zanzibar





