Winga wa zamani wa Simba Luis Miquissone yuko mbioni kujiunga na klabu ya Ken Gold ya mkoani Mbeya, imefahamika
Miquissone tayari yuko Mbeya ambapo jana alishiriki mazoezi na kikosi cha Ken Gold ambacho kimekuwa busy katika dirisha dogo la usajili kujiimarisha
Mbali na Miquissone, wachezaji wengine wanaotajwa kujiunga na timu hiyo kuinusuru isishuke daraja ni Bernard Morisson na Obrey Chirwa waliowahi kuzitumikia klabu za Yanga na Simba pia
Mabosi wa Ken Gold wamepania kuinusuru timu hiyo kushuka daraja, sasa ikiwa mkiani wa msimamo wa ligi ikikusanya alama 6 tu kutoka mechi 16



