Miquissone kuibukia Ken Gold

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th January 2025


Miquissone kuibukia Ken Gold

Winga wa zamani wa Simba Luis Miquissone yuko mbioni kujiunga na klabu ya Ken Gold ya mkoani Mbeya, imefahamika

Miquissone tayari yuko Mbeya ambapo jana alishiriki mazoezi na kikosi cha Ken Gold ambacho kimekuwa busy katika dirisha dogo la usajili kujiimarisha

Mbali na Miquissone, wachezaji wengine wanaotajwa kujiunga na timu hiyo kuinusuru isishuke daraja ni Bernard Morisson na Obrey Chirwa waliowahi kuzitumikia klabu za Yanga na Simba pia

Mabosi wa Ken Gold wamepania kuinusuru timu hiyo kushuka daraja, sasa ikiwa mkiani wa msimamo wa ligi ikikusanya alama 6 tu kutoka mechi 16


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.