CHAN 2025 yapigwa kalenda hadi August 2025

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th January 2025


CHAN 2025 yapigwa kalenda hadi August 2025

Shirikisho la Soka barani Afrika CAF limetangaza kuisogeza mbele michuano ya mataifa bingwa ya Afrika CHAN hadi Agosti mwaka huu

Taarifa ya shirikisho hilo imebainisha kwamba wameahirisha michuano hiyo licha ya waandaaji ambao ni Kenya, Tanzania na Uganda kufanya vema katika maboresho ya viwanja, hoteli, hospitali na miundombinu na vifaa vingine kwa ajili ya kuandaa michuano hiyo

Hata hivyo wataalam wa Ufundi na Miundombinu wa CAF ambao baadhi yao wapo kwenye nchi hizo za Afrika Mashariki wamelishauri shirikisho hilo kuwa muda zaidi unahitajika kuhakikisha miundombinu na vifaa vipo kwenye viwango vinavyohitajika zaidi ili michuano hiyo ifanikiwe ipasavyo

Rais wa CAF, Dk Patrice Motsepe amewashukuru Marais William Ruto wa Kenya, Dk Samia Suluhu Hassan wa Tanzania na Yoweri Museveni wa Uganda kwa uongozi wao, kujitolea na maendeleo mazuri yaliyofikiwa hasa kwenye ujenzi wa miundombinu

Licha ya michuano hiyo kusogezwa mbele shughuli ya upangaji wa ratiba ya michuano hiyo itafanyika kesho kuanzia saa 2:00 usiku Mjini Nairob, Kenya lakini tarehe rasmi ya kuanza michuano hiyo itatajwa baadae


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.