Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema mechi dhidi ya MC Alger ni ngumu hivyo wanapaswa kuendea mchezo huo kwa tahadhari kubwa
Kamwe amesema mijadala mingi inayoendeshwa huko mitandaoni inaonesha kama Yanga inakwenda kushinda kirahisi na kutinga robo fainali lakini sivyo
"Tumeona mijadala mbalimbali katika magrupu ya Whatsapp, inaonekana mashabiki wa Yanga wanaona kama mchezo dhidi ya MC Alger ni mwepesi na tunaenda kumpiga mwarabu kirahisi"
"Lakini niwaambie mechi hii ni ngumu sana tunapaswa tujiandae sawa sawa na tujitokeze kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa kuwapa hamasa wachezaji wetu"
"wakati tunacheza mchezo wa fainali kombe la Shirikisho dhidi ya USM Alger, tuliamini mechi ya hapa nyumbani ingekuwa nyepesi na tungeshinda kirahisi"
"Wapinzani wetu wakatumia kujiamini kwetu kulikopitiliza na kutuadhibu hapa nyumbani hivyo hatupaswi kurudia makosa"
"Yanga inawahitaji mashabiki 60,000 katika uwanja wa Benjamin Mkapa Jumamosi. Itakuwa ni aibu kama tutashindwa kutumia nafasi yetu nyumbani kujaza uwanja"
"Ni jukumu la kila shabiki na mwanachama wa Yanga kwenda vituoni kukata tiketi lakini pia ni jukumu la kila Mwanayanga kushiriki kuiombea dua timu yetu ili iweze kushinda mchezo huo," alisema Kamwe