Mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah, 32, anatazamiwa kupewa ofa ya pauni milioni 65 ili kumshawishi kuondoka Liverpool kuelekea Saudi Arabia msimu wa joto. (Sun)
Real Madrid wameachana na harakati zao za kumnasa mlinzi wa Liverpool Trent Alexander-Arnold, 26, na watarejea kumchukua mlinzi huyo wa Uingereza msimu wa joto. (Relevo)
Arsenal wanafikiria chaguo la kuimarisha safu yao ya ushambuliaji huku mshambuliaji wa Sporting na Uswidi Viktor Gyokeres, 26, na mshambuliaji wa Brentford wa Cameroon Bryan Mbeumo, 25, wakiwa kwenye orodha yao. (L'Equipe)
Napoli wako tayari kujiunga na kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa England na Manchester United Marcus Rashford, 27. (Sun)
Napoli pia wana uhakika wa kumsajili Alejandro Garnacho, 20, kutoka Manchester United na wamempa winga huyo wa Argentina kandarasi ya miaka mitano. (Mattino)
Hata hivyo, timu hiyo ya Serie A itakabiliana na ushindani kutoka kwa Tottenham kwa Garnacho. (Football Transfers)
Brighton wameonesha nia ya kumnunua mlinzi wa kati wa Uingereza Tosin Adarabioyo, 27, ambaye alijiunga na Chelsea mwezi Julai. (Mail)
Deportivo La Coruna wamekataa ofa kutoka kwa Chelsea kwa winga wa Uhispania Yeremay Hernandez, 22. (Metro)
City Football Group, kampuni mama ya Manchester City, iko kwenye mazungumzo ya kumsajili Juma Bah, 18, ambaye yuko kwa mkopo Real Valladolid kutoka AIK Freetong, nchini kwao Sierra Leone. (ESPN)
West Ham wanataka kupunguza hasara kwa Mbrazil Luis Guilherme, 18, na kumuuza mshambuliaji huyo miezi saba tu baada ya kumsajili. (Times)
Manchester United wamefanya mazungumzo na vilabu kadhaa, ikiwa ni pamoja na Real Betis, wakati wakijaribu kumtoa winga wa Brazil Antony mwenye umri wa miaka 24 mwezi huu. (Sun)
Chelsea hawana uwezekano wa kumsajili beki wa Uingereza Marc Guehi, 24, kutoka Crystal Palace mwezi huu baada ya kumrejesha Trevoh Chalobah, 25, kutoka Selhurst Park alikokuwa kwa mkopo. (Mail)
Newcastle wamekataa dau la pauni milioni 11 kutoka Fenerbahce kwa ajili ya kumnunua mlinzi wa Uingereza Lloyd Kelly, 26
Aston Villa imeanza mazungumzo na kiungo wa kati wa Uingereza Louie Barry, 21, kuhusu kandarasi mpya huku Celtic ikimwita. (Football Insider)
Mlinzi wa kati wa Chelsea na Ufaransa Axel Disasi, 26, anavutiwa na Juventus, Atalanta na Bayer Leverkusen. (Caught Offside)
West Ham wanataka kumleta mshambuliaji wa Nottingham Forest wa Nigeria Taiwo Awoniyi, 27. (Florian Plettenberg)
Atlanta United ya MLS inatumai kuungana tena na kiungo wa kati wa Paraguay Miguel Almiron, 30, na wanaweza kuilipa Newcastle pauni milioni 11. (Athletic)
Aston Villa wamefuatiliwa na Galatasaray kuhusu uwezekano wa kumnunua Mbrazil Diego Carlos, 31. (Fabrizio Romano)
Celtic wanakaribia kukubaliana masharti ya awali ya kandarasi na beki wa kushoto wa Arsenal wa Scotland Kieran Tierney, 27, ambaye mkataba wake unaisha mwishoni mwa msimu huu. Mabingwa hao wa Scotland pia wanatafuta kumsajili kwa mkopo mwezi huu. (Sky Sports)
BBC



