Simba imekamilisha mpango wake wa kumaliza nafasi ya kwanza hatua ya makundi kombe la Shirikisho (CAF CC) baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya CS Constantine katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Mabao ya kipindi cha pili yaliyofungwa na Kibu Denis na Lionel Ateba yalitosha kuihakikishia Simba alama tatu muhimu ambazo zinawafanya waongoze kundi A baada ya kufikisha alama 13 na kuipiku CS Constantine iliyoshuka nafasi ya pili ikiwa na alama 12
Pengine Simba ilistahili kupata ushindi mnono zaidi kama Jean Charles Ahoua na Elie Mpanzu wangetumia vyema nafasi adimu walizopata katika mchezo huo
Mnyama alitawala kwa dakika zote 90, na kuendelea kudhihrisha sasa Simba iko tayari kulileta kombe la Shirikisho Tanzania
Ushindi huo unamaanisha Simba itacheza mechi ya kwanza ugenini katika hatua ya robo fainali dhidi ya timu itakayomaliza nafasi ya pili katika kundi jingine
Milioni 10 za goli la Mama pia zimesoma katika akaunti ya Simba baada ya kufunga mabao mawili leo



