Local,Transfer News,Tabora, Singida

Mpepo alivyoikacha Tabora United kutua Singida BS

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Jan 2025
Mpepo alivyoikacha Tabora United kutua Singida BS

Mshambuliaji mpya wa Singida Black Stars, Eliuter Mpepo amefichua kilichomkwamisha kutua Tabora United katika dirisha la usajili la Januari kuwa ni kuchelewa kuwekewa dau la usajili jambo lililomfanya kubadili uamuzi licha ya kupewa mkataba wa awali

Mpepo ambaye ni mmoja wa wachezaji wa Singida Black Stars inayonolewa na Hamdi Miloud, alisema kuchelewa kwa usajili kulimfanya kuangalia fursa nyingine baada ya kupewa ofa kutoka klabu tofauti

Mchezaji huyo ambaye aliwahi kuchezea Trident ya Zambia alikofunga mabao saba na kutoa asisti tano alieleza kuwa aliona ni bora ajiunge na Singida Black Stars

"Nilikuwa na mazungumzo na Tabora United na walikuwa wanataka kunisajili, lakini kutokana na kuchelewa kuweka dau langu nilikuwa na fursa nyingine nzuri," alisema

"Niliamua kuchukua hatua ya kuhamia Singida Black Stars kwa sababu niliona ni sehemu bora kuendelea kuonyesha uwezo. Hapa nipo na furaha na najiandaa kutoa mchango mkubwa kwenye timu hii," alisema Mpepo

Mpepo ameunga na mshambuliaji raia wa Ghana Jonathan Sowah ambaye pia amesajiliwa na Singida Black Stars katika dirisha dogo

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
37m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’