Klabu ya Mashujaa imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na aliyekuwa mchezaji wao, Ismail Mgunda
Kupitia taarifa waliyotoa katika ukurasa wao wa mtandao wa kijamii, Mashujaa wamethibitisha kuondoka kwa Mgunda huku wakimtakia kila la kheri katika majukumu yake mapya
"Asante sana shujaa wetu kwa kipindi chote tulichokuwa pamoja kwenye himaya hii ya Watanganyika. Kila la kheri kwenye majukumu yako mapya," waliandika Mashujaa Fc
Mgunda anatarajiwa kujiunga na klabu ya AS Vita ya Congo DRC inayonolewa na aliyekuwa kocha wa Azam, Youssouph Dabo
Nyota huyo alikuwa DR Congo wiki chache zilizopita, Mashujaa Fc walimrejesha nchini wakati mazungumzo baina ya timu hizo yakiendelea
Inaelezwa makubaliano ya kimaslahi baina ya Mashujaa na AS Vita yamekwenda vizuri hivyo dili la Mgunda limekamilika



