Kiungo mshambuliaji wa Yanga Maxi Nzengeli amesema hana muda wa kufuatilia yanayozushwa kuhusu mkataba wake na Yanga kwani hilo sio jukumu lake
Akiwa katika msimu wake wa pili na Yanga, tayari tetesi zimeanza kuhusu hatma yake baadhi ya taarifa zikidai hatasaini mkataba mpya huku wengine wakidai mchezaji huyo anaitumikia Yanga kwa mkopo kutoka AS Maniema
Imekuwa ni kawaida kwa wachezaji wa DR Congo wanaoitumikia Yanga kuzushiwa kuwa wanacheza kwa mkopo. Ilikuwa hivyo kwa mshambuliaji wa zamani wa mabingwa hao wa nchi Fiston Mayele ambaye kwa sasa anaitumikia Pyramids Fc
Maxi amesisitiza yeye ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kutimiza majukumu yake kama mwajiriwa wa Yanga
"Kwanza niseme wazi, mimi sihusiki na tetesi, hayo ni mambo yenu nyie Wanahabari ili muuze habari"
"Pili mimi nafanya kazi yangu kama mwajiriwa wa Yanga. Kama niko hapa kwa mkopo mimi silijui hilo na wala sitaki kujua nilinunuliwa pia sijui"
"Niulize swali kuhusu majukumu yangu ndani ya Yanga, Kitu kikubwa ninachokiwaza je kocha atanipa nafasi Jumamosi niweze kuitetea nembo ya mwajiri wangu Yanga? Niulize hilo swali," alisema Maxi
Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Yanga ni kuwa makubaliano ya kuhuisha mkataba wa Maxi yamefikiwa, ni suala la muda tu Yanga itatangaza kumuongeza mkataba mchezaji huyo kiraka