Kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba ambao utapigwa Jumapili Februari 02 katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, klabu ya Tabora United huenda ikashindwa kuwatumia nyota wapya waliowasajiliwa na timu hiyo katika dirisha dogo kutokana na kukosa leseni
Imeelezwa Tabora United bado haijalipa Tsh Milioni 20 kwa ajili ya wachezaji hao 7 kupatiwa leseni
Wachezaji waliosajiliwa na Tabora United kwenye dirisha dogo ni Jean Noel, Akandwanaho, Cedric Zemba, Mwanengo, Fikirini Bakari, Chobwedo Ramadhan na Yasin Mustafa
Walina asali hao kutoka mkoani Tabora wanaweza kukumbana na changamoto kama waliyokumbana nayo duru ya kwanza katika mchezo dhidi ya Simba ambapo waliwakosa nyota wao wote wa kigeni kutokana na changamoto kama hiyo ya leseni
Hata hivyo angalau wakati huu wana uhakika wa kupata huduma ya nyota wao wengine waliobaki kikosini kwani wachezaji ambao hawana leseni ni wale waliosajiliwa kwenye dirisha dogo