Kikosi cha Simba kinaelekea mkoani Tabora leo tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tabora United ambao utapigwa kesho Jumapili, Februari 2 katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi
Simba inaelekea Tabora baada ya kukamilisha maandalizi ya mchezo huo jijini Dar es salaam
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali akiwa ameanzia mkoani Dodoma kushiriki Bunge Bonanza 2025, amesema Simba inakwenda Tabora ikiwa na kikosi kamili
Ahmed amesema Simba inazihitaji alama zote tatu ili kuendelea kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi
Baada ya mchezo dhidi ya Tabora United, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Manyara kuikabili Fountain Gate Februari 6



