Simba kuifuata Tabora United leo, yapania ushindi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st February 2025


Simba kuifuata Tabora United leo, yapania ushindi

Kikosi cha Simba kinaelekea mkoani Tabora leo tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tabora United ambao utapigwa kesho Jumapili, Februari 2 katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi

Simba inaelekea Tabora baada ya kukamilisha maandalizi ya mchezo huo jijini Dar es salaam

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali akiwa ameanzia mkoani Dodoma kushiriki Bunge Bonanza 2025, amesema Simba inakwenda Tabora ikiwa na kikosi kamili

Ahmed amesema Simba inazihitaji alama zote tatu ili kuendelea kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi

Baada ya mchezo dhidi ya Tabora United, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Manyara kuikabili Fountain Gate Februari 6


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.