Arsenal yaisambaratisha Manchester City Emirates

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd February 2025


Arsenal yaisambaratisha Manchester City Emirates

Arsenal imefufua matumaini katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuwachapa wapinzani wao Manchester City mabao 5-1 Jumapili usiku

Ni kipigo cha aibu ambacho kinawafanya The Gunners kulipiza kisasi dhidi ya mabingwa hao

Mvutano kati ya timu hizo ulikuwa mkubwa baada ya sare ya 2-2 Septemba lakini hatimaye Arsenal wamepata ushindi dhidi ya vijana wa Pep Guardiola, ambao walikuwa wamebeba ubingwa katika misimu miwili iliyopita

Mabao kutoka kwa vijana Myles Lewis-Skelly na Ethan Nwaneri yalihakikisha ushindi wa kishindo kwa kikosi cha Mikel Arteta, baada ya Martin Odegaard kuwafungia Arsenal mapema ndani ya dakika mbili

Erling Haaland alisawazisha katika kipindi cha pili lakini Arsenal walirudisha faida yao ndani ya sekunde 38 baada ya kuanza tena bao la Thomas Partey likimpita John Stones

Lewis-Skelly aliongeza dakika tatu baadaye likiwa bao lake la kwanza la Arsenal, kabla ya kuonekana kumdhihaki Haaland kwa kunakili aina yake ya ushangiliaji

Kai Havertz alifunga bao la nne kabla ya Nwaneri kuingia akitokea benchi kukamilisha kipigo cha aibu kwa mabingwa hao na kupunguza uongozi wa Liverpool kileleni mwa jedwali

Arsenal imefikisha alama 50 katika nafasi ya pili Liverpool wakiwa kileleni na alama 56


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.