Arsenal imefufua matumaini katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuwachapa wapinzani wao Manchester City mabao 5-1 Jumapili usiku
Ni kipigo cha aibu ambacho kinawafanya The Gunners kulipiza kisasi dhidi ya mabingwa hao
Mvutano kati ya timu hizo ulikuwa mkubwa baada ya sare ya 2-2 Septemba lakini hatimaye Arsenal wamepata ushindi dhidi ya vijana wa Pep Guardiola, ambao walikuwa wamebeba ubingwa katika misimu miwili iliyopita
Mabao kutoka kwa vijana Myles Lewis-Skelly na Ethan Nwaneri yalihakikisha ushindi wa kishindo kwa kikosi cha Mikel Arteta, baada ya Martin Odegaard kuwafungia Arsenal mapema ndani ya dakika mbili
Erling Haaland alisawazisha katika kipindi cha pili lakini Arsenal walirudisha faida yao ndani ya sekunde 38 baada ya kuanza tena bao la Thomas Partey likimpita John Stones
Lewis-Skelly aliongeza dakika tatu baadaye likiwa bao lake la kwanza la Arsenal, kabla ya kuonekana kumdhihaki Haaland kwa kunakili aina yake ya ushangiliaji
Kai Havertz alifunga bao la nne kabla ya Nwaneri kuingia akitokea benchi kukamilisha kipigo cha aibu kwa mabingwa hao na kupunguza uongozi wa Liverpool kileleni mwa jedwali
Arsenal imefikisha alama 50 katika nafasi ya pili Liverpool wakiwa kileleni na alama 56



