Baada ya mapumziko ya siku chache, kikosi cha Simba kilirejea mazoezini jana kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa kesho Jumanne, Februari 11 katika uwanja wa KMC Complex
Baada ya kudondosha alama mbili kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo uliopita, ni wazi Simba inapiga hesabu za kushinda mchezo huo ili kuendelea kubaki katika eneo salama kwenye mbio za ubingwa
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema Kwa sasa hawana tena nafasi ya kudondosha alama iwe nyumbani au ugenini kwenye 'ngwe' hii ya lala salama
"Ni kweli, tumerejea uwanja wa mazoezi kujiandaa na mchezo dhidi ya Tanzania Prison Jumanne February 11 katika Uwanja wa KMC. Focus yetu kwa sasa ni kupata ushindi katika mchezo huo," alisema Ahmed



