KenGold yafufua matumaini kubaki Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th February 2025


KenGold yafufua matumaini kubaki Ligi Kuu

Ken Gold imeendelea kuweka hai matumaini ya kubaki ligi kuu msimu huu baada ya kuichapa Kagera Sugar bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sokoine

Ni ushindi wa pili kwa KenGold katika mechi nne zilizopita ambao wachimba dhahabu hao wamevuna alama 7 kati ya alama 12

KenGold imefikisha alama 13, sasa ikihitaji alama nne ili kuondoka katika eneo la kushuka daraja

Unaweza kusema usajili uliofanywa na marajiri hao kutoka Mbya katika dirisha dogo wakisajili wachezaji 24, umebadili upepo

Nayo KMC imepoteza mechi ya pili mfululizo katika uwanja wa KMC Complex ikichapwa mabao 2-0 na JKT Tanzania


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.