Ken Gold imeendelea kuweka hai matumaini ya kubaki ligi kuu msimu huu baada ya kuichapa Kagera Sugar bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sokoine
Ni ushindi wa pili kwa KenGold katika mechi nne zilizopita ambao wachimba dhahabu hao wamevuna alama 7 kati ya alama 12
KenGold imefikisha alama 13, sasa ikihitaji alama nne ili kuondoka katika eneo la kushuka daraja
Unaweza kusema usajili uliofanywa na marajiri hao kutoka Mbya katika dirisha dogo wakisajili wachezaji 24, umebadili upepo
Nayo KMC imepoteza mechi ya pili mfululizo katika uwanja wa KMC Complex ikichapwa mabao 2-0 na JKT Tanzania



