Mchezo wa ligi kuu kati ya Simba dhidi ya Azam Fc uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa umemalizika kwa matokeo ya sare ya mabao 2-2
Ni Mzizima Derby, mechi kali iliyokuwa na upinzani kutoka kwa kila upande, Simba wakitawala mchezo huku Azam Fc wakitumia mashambulizi ya kushitukiza
Azam Fc walitangulia kufunga bao la uongozi mapema dakika ya kwanza Gibril Sillah akimalizia shambulizi la kushitukiza
Elie Mpanzu aliirejesha Simba mchezoni dakika ya 25 akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Kibu Denis
Kipindi cha pili Simba iliendelea kupeleka mashambulizi langoni kwa Azam Fc na ikafanikiwa kufunga bao la pili dakikaa ya 76 Abdulrazak Hamza akimalizia kwa kichwa mipra wa adhabu uliopigwa na Jean Charles Ahoua
Hata hivyo Azam Fc walirejesha bao hilo dakika 2 kabla ya mchezo kumalizika Zidane Sereli akifunga baada ya pasi ya Feisal Salum baada ya kumzidi mbio nahodha Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr'



