Baada ya mfululizo wa vipigo vizito katika ligi kuu ya NBC, klabu ya Mashujaa Fc imetangaza kusitisha mkataba wa kocha mkuu Mohammed Abdallah 'Barres'
Jana Mashujaa Fc ilikumbana na kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Singida Black Blacks kikiwa ni kipigo cha pili mfululizo baada ya kuchapwa mabao 5-0 na Yanga katika mchezo uliopita
Katika mechi 12 zilizopita, Mashujaa Fc iliambulia ushindi katika mchezo mmoja tu dhidi ya Pamba Jiji




