Mashujaa Fc yaachana na Barres

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th February 2025


Mashujaa Fc yaachana na Barres

Baada ya mfululizo wa vipigo vizito katika ligi kuu ya NBC, klabu ya Mashujaa Fc imetangaza kusitisha mkataba wa kocha mkuu Mohammed Abdallah 'Barres'

Jana Mashujaa Fc ilikumbana na kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Singida Black Blacks kikiwa ni kipigo cha pili mfululizo baada ya kuchapwa mabao 5-0 na Yanga katika mchezo uliopita

Katika mechi 12 zilizopita, Mashujaa Fc iliambulia ushindi katika mchezo mmoja tu dhidi ya Pamba Jiji


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.