Kocha Msaidizi wa Simba Selemani Matola amesema maandalizi yao kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union yamekamilika
Matola amesema wanatambua mchezo huo utakuwa mgumu lakini anaamini maandalizi mazuri waliyofanya yatawapa nafasi ya kushinda mchezo huo
Nahodha huyo wa zamani wa Simba amesema mechi zote za duru ya pili ni ngumu hivyo jambo muhimu kwao ni kupambana kila mechi ili kupata matokeo
"Mechi zote za mzunguuko wa pili ni ngumu hivyo tunatarajia hata mchezo wa kesho (leo) dhidi ya Coastal Union utakuwa mgumu"
"Hata hivyo tumekuwa na maandalizi mazuri kuelekea mchezo huo, nina imani kubwa tutakwenda kushinda mchezo huu," alisema Matola
Nae nahodha wa Simba Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr' amesema wako mkoani Arusha kwa kazi moja tu, kuchukua alama tatu dhidi ya Coastal Union
"Tumekuja kwenye mchezo huu wa ugenini kutafuta pointi tatu, hilo ndio jambo muhimu pasipo kuangalia matokeo ya mechi zilizopita kwani yameshapita," alisema Zimbwe Jr